Gari lililobeba mwili wa Mangweha baada ya kuwasili mkoani Morogoro.
Wakazi wa Moro waliofika kuupokea mwili wa Mangweha.…
Umati wa watu ukisubiri msafara wenye mwili wa marehemu Mangweha.
Mwili wa msanii mahiri wa
muziki wa kizazi kipya, Albert Kenneth Mangweha, umewasili mkoani
Morogoro jioni hii. Mangweha alifariki dunia ghafla Jumanne ya Mei 28
mwaka huu huko nchini Afrika Kusini. Msanii huyo anatarajiwa kuzikwa
kesho katika makaburi ya Kihonda jirani na alipozikwa baba yake mzazi.
Kabla ya mazishi kutakuwa na ibada ya kumwombea marehemu pamoja na zoezi
la kuaga mwili kwa wakzi wa Morogoro.
No comments:
Post a Comment