WAREMBO wanne jana wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Sokoine
Drive (Jiji) jijini Dar es Salaam kwa kosa la kunywa pombe za kienyeji
muda wa kazi.
Warembo hao walinaswa maeneo ya Pugu nje kidogo ya
jiji la Dar es Salaam. Baada ya kufikishwa mahakamani hapo na kukana
mashitaka hakimu aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo, Timothy Lyon,
aliwawekea wazi dhamana kwa kumtaka kila mmoja kuwa na wadhamini wawili
na dhamana ya shilingi laki mbili kila mmoja. Sharti hilo la dhamana
lilikuwa gumu kwa warembo hao ambao walipandishwa karandinga na
kupelekwa Gereza la Segerea mpaka tarehe 15 mwezi ujao.
PICHA : RICHARD BUKOS / GPL
No comments:
Post a Comment