Saturday, August 10, 2013

HIKI NDICHO KILICHO WAKUTA MWANA FA NA AY MADAWA YA KULEVYA


Itakumbukwa kama wiki mbili zimepita tangu msanii wa Bongo Flava, Madee kusema kua alipofika nchini Afrika Kusini alifanyiwa parapata ya kutosha kuhakikikisha kua hajabeba madawa ya kulevya. Alisema ilibidi avulishwe hadi nguo ili jamaa waendelee na ukaguzi wao.

Sasa jana ishu ya kukaguliwa imewakuta Mwana FA na AY pale walipowasili kwani nao walikaguliwa sana tu ili kuhakikisha kua hawajabeba mzigo aka Sembe. Kupitia mtandao wake wa Twitter Mwana FA aliandikwa tweet hii kuhusu ukaguzi huo.

hawa watu walivyotupekua na mwanangu @AyTanzania na kutu'treat kama wana UHAKIKA tumebeba hizo 'ngano' zao hapa JNIA..nimevunjika moyo SANA.
— Hamis Mwinjuma (@MwanaFA) August 9, 2013

Na mda mfupi tu baada ya kuandika tweet hiyo haya ndo yalikua majibu ya Followers wake akiwemo Flaviana Matata, AY na wengine wengi, cheki hapa chini


No comments:

Post a Comment