Thursday, July 18, 2013

WABONGOMWANAO KAMATWA NA UNGA NJE IDADI YAO

Akizungumza ofisini kwake Dar es Salaam leo Kamishina wa Tume ya Kuratibu na Kuthibiti Dawa za Kulevya nchini, Christopher Shekiondo alisema kwamba inaonesha Watanzania wengi wamekamatwa na dawa za kulevya nchini Brazil ambao idadi yao inafikia 109, ambapo wengi wao wameshahukumiwa.

Alisema watu hao wamekamtwa nchini humo, wakiwa na dawa aina ya cocain kwa ajili ya kusafirisha nchi nyingine, huku baadhi yao wamehukumiwa kunyongwa pamoja na kifungo cha maisha, ingawa idadi kamili ya watu hao bado haijafika rasmi.

"Tumepokea taarifa jumla ya Watanzania 109 wamekamtwa nchini Brazil, ingawa bado tunasubiri kujua ni wangapi waliohukumiwa kifo, pamoja na kifungo cha maisha," alisema Shekiondo.

Aliongezea kuwa baadhi ya nchi nyingine, ambazo Watanzania wanakamatwa na dawa hizo za kulevya wakiwa wanasafirisha ni China vijana 34, Kenya 30, Pakistani 16, Falme za Kiarabu ikiwemo Dubai 14,  pamoja na nchi nyingine kama Japan, Argentina, Msumbiji, Afrika Kusini, Ureno, pamoja na Uingereza.

Akizungumzia hukumu ambazo zimeshatolewa baadhi ya nchi walizokamatwa Watanzania hao,, Kamishina huyo alisema Brazil ambayo ndiyo Watanzania wengi wamekamatwa idadi kamili, bado hawajapata ingawa Kenya tayari wapo waliohukumiwa kifungo cha maisha, huku wengine wakiwa wamehukumiwa kifungo cha miaka 20 hadi 40, nchi China wapo waliohukumiwa kifo na kifungo cha maisha.

Shekiondo alisema Tanzania kwa sasa inajulikana kama ni njia ya kusafirisha dawa hizo.

Alisema kuna baadhi ya watu wanatumia maji kusafirisha dawa hizo, yaani meli, jahazi pamoja na mitumbwi, hivyo wana mikakati ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu udhibiti wa matumizi ya dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment