wadau, habari zenye uhakika kutoka katavi national park ninathibitisha kuwa basi la summry kutoka mbeya kuelekea mpanda - katavi lilitumbukia kwenye mto maarufu pale mbugani kama shule ya viboko. Mpaka ninavyoandika saa 4.00 asubuhi hii ya ijumaa 5/7/2013 maiti mbili ziko hospital mpanda na maiti sita zimeopolewa toka mtoni. Maiti zaidi zikipatikana tutawajuza. Poleni majeruhi, poleni wafiwa.

Basi lilitumbukia mnamo saa 8: 16 usiku
dereva alipitia njia illiyokatazwa na serikali so aliiba njia.
Basi lilijaza kupita maelezo, kumbuka ni wakati wa mavuno kwahiyo watu wanasafiri sana
kumbuka hii njia ni summry pekee anayefanya biashara, akija kampuni nyingine anawapiga majuju hadi wanahama.... Wafipa wanajua anachofanya summry.
Mto ambao basi limetumbikia ni maarufu kwa ajali kama hizo.