Tukio 
hilo lilitokea mwanzoni mwa wiki ambapo imeelezwa kuwa Nkamia mbali na 
kutaka kumpiga mbunge huyo, pia alimtolea matusi mazito ya nguoni 
(gazeti hili haliwezi kuandika).
Kwa mara 
ya kwanza mbunge huyo aliingia katika kashfa baada ya kutoa kauli 
bungeni kuwa hazungumzi na mbwa, bali anazungumza na mwenye mbwa kabla 
ya kuingia katika mzozo na wahariri na baraza la habari aliposema kuwa 
Jukwaa la Wahariri na Baraza la Habari ni NGOs za kutafuta fedha.
Uchunguzi
 wa Mwananchi ambao umethibitishwa na Nkamia mwenyewe umebaini kuwa 
chanzo cha tukio hilo ni kutokana na kuzomewa kwa Nkamia katika kampeni 
za uchaguzi mdogo Kata ya Dalai Wilaya ya Chemba.
Kwa 
mujibu wa wabunge mashuhuda ambao waliliona tukio hilo, ilielezwa kuwa 
Nkamia, ambaye pia ni mwandishi wa habari, alianza kumshushia matusi 
Moza wakiwa ndani ya Bunge hadi walipotoka nje alimfuata na kutaka 
kumpiga.
"Kweli 
pale jamaa yetu, alitia aibu, hata hivyo kusema kuwa alikuwa amelewa 
siyo kweli maana mimi namfahamu Nkamia vizuri ila ilikuwa ni hasira tu,"
 alisema mmoja wa wabunge walioamua ugomvi huo.
Akizungumzia
 tukio hilo Moza, alisema kuwa wakati akitoka nje ya ukumbi, alipita 
karibu na kiti anachokaa Nkamia na ghafla akaitwa, lakini akashangazwa 
na kitendo cha kuanza kurushiwa matusi.
"Kweli 
Nkamia na mimi tunatoka wilaya moja, lakini siku ile nilishangaa 
alinitukana matusi ya nguoni kabisa ......... (anayataja), lakini mimi 
kule sikusema kitu hadi nilipotoka nje alinifuata na mimi hasira 
ilinishika nikaanza kumjibu akatupa vitabu ili aje anipige wabunge 
wenzake wakamkamata," alisema Moza.
Alisema 
kuwa chanzo cha matusi hayo ilikuwa ni tuhuma kwamba Nkamia alimtuhumu 
Moza kuwa aliandaa vijana katika Kata ya Dalai wakati wa kampeni za 
uchaguzi wa udiwani ili wamtukane.
"Hata 
hivyo, waliomwambia hivyo kwamba niliandaa vijana au nilimtukana 
walimdanganya kwani mimi wakati huo nilikuwa bungeni, lakini yeye ndiye 
aliyeniporomoshea matusi katika kampeni hizo na ushahidi wa sauti 
ninao," alisisitiza Moza.
Kwa 
upande wake Nkamia, ambaye kabla ya kuwa mbunge alikuwa mtumishi wa 
Serikali katika Shirika la Tanzania Broadcasting Corporation (TBC) 
alikiri kutokea kwa tukio hilo, lakini alikanusha kuingia bungeni akiwa 
amelewa kama ilivyoaminika na watu.
Nkamia 
alitoa sababu za ugomvi huo kuwa ni kutokana na taarifa kuwa Moza 
aliandaa kikosi cha vijana wahuni kulishambulia gari la Chama Cha 
Mapinduzi (CCM) pamoja na kuwazomea viongozi wake akiwemo yeye.
No comments:
Post a Comment