Maeneo ya Makorongoni yakiwa yametanda moshi mzito
POlisi wakilinda barabara ya Iringa - Dodoma ambayo ilitekwa na wamachinga hao na kuchoma mataili barabarani
Wananchi wakiwa juu ya nyumba zao kushuhudia matukio
Hali bado yaendelea kwenda kombo katika Manispaa ya Iringa baada ya askari polisi kukamata watu zaidi ya 50 akiwemo aliyekuwa mgombea udiwani kata ya Kwakilosa na kampeni meneja wa Chadema jimbo la Iringa mjini Abuu Majeck
Hadi sasa biashara katika mji mzima zimesimama na polisi wameendelea kuweka sawa ulinzi katika mitaa mbali mbali .
Kwa sasa baadhi ya mitaa ya mji wa Iringa imetanda moshi uliotokana na mataili yaliyochomwa na machinga hao.
Taarifa za sasa kutoka jeshi la polisi ni kwamba mbunge wa jimbo hilo mchungaji Peter Msigwa (Chadema) ambae anadaiwa kuwa chanzo cha vurugu hizo anasakwa japo mtandao huu nusu saa iliyopita ulimshuhudia akiwa eneo la chuo cha Tumaini katika harambee inayoendeshwa na waziri mkuu wa zamani Mh. Sumaye .
Mbunge mchungaji Peter Msigwa |
Polisi waliotoka kumkamata mbunge Msigwa leo |
Gari ya mbunge Msigwa kabla ya kukamatwa leo kwa kuhusishwa na vurugu ..........................................................................................
Na Francis Godwin, Iringa
MASAA zaidi ya 6 ya
mapambano kupiga mabomu ya machozi na
kurushiana mawe kati ya
wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga ) na askari
wa kikosi cha kutuliza
ghasia (FFU) mkoani Iringa
yaishia pabaya kwa jeshi la
polisi kumkamata mbunge wa
jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (chadema) na
watu wengine zaidi ya 60
Polisi watumia mabom ya machozi kutawanya machinga wapiga mabomu hadi stendi kuu ya mabasi abiria
walazimika kutimua mbinu na kuacha mizigo yao katika magari huku machinga hao wakitumia mawe na kuchoma mataili moto barabarani kuvunja vioo vya gari la Zimamoto na kuharibu mali mbali mbali kama njia ya
kupambana na polisi
Tukio hilo la Mapambano kati ya machinga na polisi lilitokea leo kuanzia muda wa saa 3 asubuhi
na kuendelea hadi saa 8 mchana katika eneo la Mashine tatu
mjini Iringa na maeneo mbali
mbali ya mji wa Iringa .
Mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com
na www.matukiodaima.com ambao ulikuwepo eneo la
tukio toka saa 12
za asubuhi ya jana alishuhudia kundi kubwa la askari wa FFU wakiwa na gari la maji ya kuwasha ambao
wakesha wakilinda eneo hilo .
Askari huo walilazimika
kukesha wakilinda eneo hilo
kufuatia kauli ya mbunge
Msigwa aliyoendelea kuitoa
katika mikutano yake ya hadhara mjini hapa
kuwhamasisha machinga hao ambao
Halmashauri ya Manispa ya
Iringa iliwahamisha eneo hilo la mashine tatu na kuwapeleka
eneo la Mlandege kabla ya mbunge
Msigwa kuwahamasisha kurejea tena
eneo hilo.
Kabla ya mbunge
Msigwa kufika eneo hilo majira ya saa 3 asubuhi machinga hao ambao
walikuwa wamejikusanya makundi
madogo madogo bila kupanga
biadhaa zao walisikika wakidai
kumsubiri mbunge Msigwa kama
alivyopata kuwaahidi kuwa atafika
eneo hilo kuungana nao kwa kuwa
machinga mpya .
Hata hivyo baada ya mbunge
huyo kufika akiwa na gari lake la
kibunge ambalo lilikuwa lilikokota
tela la
kuhifadhia mizigo alisimama eneo hilo na
kuendeleza msimamo wake wa kuwataka machinga kupambana na baada ya muda alitoweka eneo hilo kabla ya polisi
kuanza kuwatawanya machinga hao kwa mabomu ya machozi .
Wakizungumzia hali
hiyo ambayo ni ya kwanza kutokea katika mji wa
Iringa wakazi wa mji wa Iringa
walisema kuwa mbunge na
viongozi wengine wa
serikali wanapaswa kulaumiwa kwa
kushindwa kutumia njia nzuri
ya kukutana kwa ajili ya kumaliza mvutano huo
ambao unaendeshwa kisiasa zaidi.
Festo Sanga
alisema kuwa hali
ilipofikia ni mbaya zaidi na hivyo
busara zinahitajika kwa ajili
ya kutatua tatizo
hilo ikiwa ni pamoja na
kutazama eneo zuri kwa ajili ya
machinga bila kuendelea
kuonyeshana ubabe .
Sanga alisema kuwa machafuko yaliyojitokeza leo ni machafuko ambayo wakazi wa mji
wa Iringa walikuwa wakishuhudia katika vyombo
vya habari katika mikoa
mingine ukiacha lile la Septemba 2 mwaka jana lililotokea kijiji
cha Nyololo kati ya wafuasi wa Chadema na polisi na kupelekea kifo cha
aliyekuwa mwenyekiti wa klabu ya
waandishi wa habari mkoa wa Iringa marehemu Daud Mwangosi.
“Kweli katika hili
mbunge wetu hapaswi kuendelea
kulazimisha machinga kuvunja sheria
ila anayo nafasi ya kukutana na
viongozi wenzake ili
kutafuta suluhu ya jambo
hilo vinginevyo wanaoteseka na
machinga na wale waliokamatwa kwa vurugu hizo
ujue wengi waliopigwa mabomu ya machozi si machinga wengine
walikuwa wasafiri na badhi
yao walikuwa wakielekea makanisani ”
KUhusu kukamatwa kwa
mbunge huyo na kuhojiwa na polisi
juu ya vurugu hizo Sanga alisema kwa upande wake analipongeza jeshi la
polisi kwa kutumia busara zaidi
ya kumkamata mbunge
kama mhusika mkuu na kuliomba
jeshi la polisi kuwaachia wananchi
waliokamatwa kwa vurugu
hizo.
Huku Sarah
Kalinga alidai kuwa
chanazo cha machafuko hayo ni mvutano kati ya CCM na Chadema na kuwa
ilipaswa vyama vyote viwili
kukutana na kuwasaidia machinga
badala ya kuwanyanyasa kwa
kutumia nguvu kuwabana .
Hata hivyo alisema wao kama walalahoi wanampongeza mbunge wao kwa kuonyesha kuwapigania japo
haungi mkono njia inayotumiwa na mbunge
ya kuwahamasisha kuvunja
sheria na kuwa matatizo na
majeraha wanapata wao
wananchi na sio mbunge.
Awali mbunge
mchungaji Msigwa kabla ya kukamatawa na
jeshi la polisi alitoweka katika
mazingira tata katika eneo hilo la mashine tatu na
kuibukia eneo la chuo kikuu cha
Tumaini Iringa ambako kulikuwa na harambee
ya kuchangia Kanisa na mgeni rasmi akiwa
waziri mkuu mstafu Frederick Sumaye na mara baada ya
shughuli hiyo kumalizika ndipo alipokamatwa na polisi na
kufikishwa kituo cha polisi.
Kabla ya
kukamatwa kwake mbunge Msigwa
alizungumza na mwandishi wa habari hizi
na kuwa yupo tayari kukamatwa wakati
wowote na kuwa kamwe ataendelea
na msimamo wake wa
kuwataka Machinga kufanya biashara
eneo hilo.
Mbali ya
kukamatwa kwa mbunge
Msigwa kwa kuhusishwa na vurugu hizo pia
jeshi la polisi mkoani Iringa
linawashikilia watu wengine
zaidi ya 60 akiwemo aliyekuwa
kampeni meneja wa Chadema jimbo la Iringa mjini na mgombea udiwani
kata ya kwa Kilosa Abuu Changawa Majeck.
Huku idadi ya
majeruhi waliojeruhiwa kwa kupigwa mawe na machinga na badhi ya machinga waliokamatwa kwa vurugu
hizo pia wakijeruhiwa vibaya wakati
wakipambana na polisi hao.
Taarifa kutoka jeshi
la polisi zilizothibitishwa na kamanda
wa polisi mkoa wa Iringa Michael
Kamuhanda zinadai kuwa
watu zaidi ya 60 ndio wamekamatwa
hadi sasa na jitihada za
kuwasaka wengine waliohusika
katika vurugu hizo ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa wa
mali za
wananchi unaendelea.
Huku akidai mali mbali mbali
zimeharibiwa likiwemo gari hilo
la zimamoto mjini Iringa pamoja na uharibifu
mwingine mdogo mdogo
wa mali za wananchi .
Jeshi hilo la
polisi limesema kamwe halipo tayari kumwachia mbunge Msigwa kwa leo hadi hapo
atakapofikishwa mahakamani Kesho
MWISHO
|
Habari ambazo zimetua hivi punde katika mtandao huu zinadai kuwa msafara wa askari wa FFU pamoja na gari la zimamoto kutoka jiji la Mbeya upo njiani kuja mjini Iringa kuongeza nguvu zaidi .
Mbunge Msigwa akisalimia katika harambee iliyoendeshwa na Sumaye leo katika chuo cha Tumaini Iringa
Watalii wakiogopa kuendelea na safari baada ya kutokea machafuko mjini Iringa
Jeshi la polisi mkoa wa Iringa limemkamata mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (Chadema) kufuatia kuhusishwa na vurugu za machinga eneo la mashine tatu hii leo
Hivi sasa mbunge huyo yupo katika kituo kikuu cha polisi mjini Iringa akihojiwa na polisi kufuatia vurugu hizo ambazo kwa sasa zimetulia na wananchi wameanza kuendelea na biashara zao.
No comments:
Post a Comment