Monday, May 13, 2013

VIONGOZI WA CHADEMA KATIKA HARAKATI MBALI MBALI WIKI HII

LISU bbf1f

 "SERIKALI dhalimu huondolewa na wenye hasira na waliochoka, kunyanyaswa na kudhulumiwa haki zao".
Hayo yamesemwa na Mbunge wa Singida Mashariki na mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni Tundu Lissu katika mkutano wa hadhara uliomalizika hivi punde katika viwanja vya Mkwawa nje kidogo na geti la Chuo Kikuu.

Lissu amesema serikali yoyote haiondolewi madarakani kwa maombi bali kwa kutumia maamuzi ya kisiasa na kwa kupiga kura za kuikataa hasa unapofika wakati wa kufanya uchaguzi.
Amesema mambo ya kikaisari yanatatuliwa kikaisari na hali lilipofikia taifa la Tanzania, ni pabaya ambapo wananchi wana kila sababu ya kukichukia chama tawala ambacho kinawatia umasikini wananchi bila sababu.
"Usije ukadanganyika kuwa ukimuomba Mungu utakuta CCM imetoka madarakani, haya ni mambo ya kikaisari ambayo yanatakiwa kutatuliwa kikaisali hivyohivyo. Usidhani ukimuomba Mungu pale utakapokuwa unamaliza sala utakuta CCM haipo, kamwe! Huu ni wakati wa kuichukia na kuiondoa, haifai tena. Ila siwaambii kama musiende kumuomba Mungu, saline lakini hakikiseheni mnachukua maamuzi ya kuiondoa CCM" amesema Lissu.
Amesema upinzani wamekuwa na hoja za kuisaidia serikali lakini kwa sababu ya ufinyu wa fikra za viongozi wa chama hicho, hoja zao zimekuwa zikipuuzwa kwa sababu ya uwingi wa watu kwa kutumia "ndiyooo!" badala ya kuangalia mwenendo mzima wa maisha ya watanzania.
"Ndugu zangu, kwenye bunge letu tuna wabunge wachache tu na wengine wengi ni kundi tu la walaji ambalo halina kazi yoyote" amesema.
Amesema CCM imegombana na kila mtanzania kwa kila nyanja kwa kuwa kila kitu kinachofanyika na serikali kinambana mwananchi.
Ameeleza kuwa serikali imeingia katika mifuko ya hifadhi ya jamii na kutumia hela za watanzania bila sababu huku ikiwanyima haki zao pale wanapostaafu.
"Kila kinachofanyika na serikali kinatumia pesa za wananchi wanaoweka pesa zao katika mifuko yao bila kuwaarufu wananchi wenyewe. Niwambieni kuwa leo hii kwa wewe unayeweka pesa zako katika mfuko wowote wa jamii pindi utakapostaafu imekula kwako hutaipata tena pesa yako kwa sababu watu wamegawana" amesema.
Amesema hakuna ambaye halalamiki juu ya kile anachotendewa na serikali awe polisi, mwalimu, machinga, mama lishe hata mwanafunzi.
Hata hivyo amesema jeshi la polisi linalotumika na baadhi ya wanasiasa wa Chama cha Mapinduzi limedhurumiwa na serikali kuliko hata machinga.
Akifafanua zaidi amesema kila wakati zimekuwa zikitolewa pesa kwa ajili ya mafunzo ya jeshi la polisi, nyongeza za mishahara, likizo na kupandishwa vyeo lakini zimekuwa zikipigwa juu kwa juu na viongozi wa chama tawala.
"Leo hii ugomvi wa wanafunzi wa vyuo vikuu na serikali ni mkopo, nchi inadaiwa na benki za nje, taasisi za fedha za nje na mashirika ya fedha, walimu na polisi pia; ni nani hajaumizwa na serikali hii dhalimu?" amesema.
Amewataka watanzania kupongezana kwa kazi ambayo imekwisha kufanyika na kuwakumbusha kuwa bado kuna kazi kubwa ipo mbele yao kuhakikisha serikali dhalimu inaondoka.
Lissu amekwenda kinyume na kauli ya Waziri William Lukuvi bungeni kuwa kamanda wa polisi Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda anafanya kazi nzuri na hivyo kumtaka aendelee na kazi hiyo kuwa inaonesha dhahiri jinsi Chama cha Mapinduzi kinavyotumia jeshi la polisi kuwakandamiza wananchi.
"Katika tume zilizoundwa kuchunguza mauaji ya mwandishi wa habari Daudi Mwangosi ikiwemo tume ya serikali ya tume ya haki za binadamu, ripoti inasema Kamuhanda Mwangosi aliuawa kwa usimamizi wa Kamuhanda na ni muuaji lakini leo hii anasimama Waziri halafu anasema Kamuhanda huyo huyo anafanya kazi nzuri! Inatisha sana" anasema.
Hata hivyo amesema Kikwete pamoja chama chake wanatambua kuwa inchi ilipofika sasa mbele ni giza tu kwa kuwa hakuna njia zinazowezakutumika kuwakomboa wananchi kwa udhalimu wao.
Lissu amesema wananchi wa hali ya chini ndiyo wanaokamuliwa kodi huku watoto wa viongozi na wafanyabiashara wakubwa wakiachwa kwa sababu ndio walioinunua serikali.
Hata hivyo mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO) Olime Mwakilembe amesema imefika mahali CCM inakata ushauri na kufanya mambo magumu kwa njia rahisi wakidhani wanatatua matatizo na badala yake kuwapa mzigo wananchi.
Amesema hali ya maisha ya watu ilipofika inatisha kwa sababu ya serikali legelege isiyo na masikio inayotumia mabavu kuwalazimisha wananchi kuingia motoni badala ya kutumia rasilimali watu kuokoa maisha ya watanzania.
"Matatizo magumu wanafanya kwa njia rahisi. Ushauri wa maana wanaukata kwa sababu ya uhuni wao wa kutumia mabavu na kuwanyanyasa wananchi ambao ndio walipa kodi wanazoendeshea maisha yao na familia zao. Uhuni huu unafanyika kwa wazi kabisa huku watanzania wakiuona" amesmea.
Amewataka watanzani kutokufumbia mamcho matatizo yanapotokea ambayo chanzo kikuu ni viongozi wanafiki waliojaa dhuruma na kujilimbikizia mali.
Hata hivyo amesema wakati wa kuiaga CCM umefika na kiama chake kimekamilika ambacho ni Chadema.
Mkutano huo uliandaliwa na shirikisho la vyuo vikuu Mkoa wa Iringa ambavyo ni Chuo Kikuu kishiriki cha Tumaini Iringa, Chuo Kikuu kishiriki cha Mkwawa na Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO).

MBOWE 7c36b
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Jimbo la Hai, Freeman Mbowe akimkabidhi nahodha wa Timu ya Mpira wa Miguu ya Wazawa FC ya KIA, Efati Mwasumbi, zawadi ya jezi na mipira kwa ajili ya timu hiyo jana. Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la chama hicho (BAVICHA) Dorice Cornel. Kiongozi huyo yuko katika ziara ya wiki mbili jimboni kwake kuzungumza na wananchi wa jimbo hilo.


chdm 6a959
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe na Mbunge wa Hai, akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa chama hicho Kijiji cha Mtakuja, Mzee Ally Mbatia. Mbowe yuko katika ziara ya kukagua uhai na kuimarisha ujenzi wa chama katika ngazi ya chini kabisa ya chama hicho, msingi, kwenye maeneo ya vitongoji mbalimbali katika vijiji vya Jimbo la Hai.

No comments:

Post a Comment