Thursday, May 2, 2013

HIVI NDIVYO BARCA ALIVYO KUFA

HAKUNA maajabu hapa. Itakuwa fainali ya Wajerumani watupu Ligi ya Mabingwa Ulaya Uwanja wa Wembley wiki tatu zijazo Jumamosi, ikiwakutanisha Bayern Munich na Borussia Dortmund.
Hiyo inafuatia Barcelona iliyomkosa Lionel Messi aliyekuwa benchi kutandikwa mabao 3-0 nyumbani usiku huu, baada ya awali kuchapwa 4-0 Ujerumani, hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 7-0.
Barcelona walionekana kabisa kuzidiwa uwezo na mapema tu walionekana hawawezi kupanda mlima huo. Mabao ya Bayern ambao tayari ni mabingwa wa Ujerumani, wakiivua taji Dortmund, yamefungwa na Arjen Robben dakika ya 49, Gerard Pique aliyejifunga dakika ya 72 na Thomas Muller dakika ya 76.
Kikosi cha Barca leo kilikuwa; Valdes, Dani Alves, Pique, Bartra/Montoya dk87, Adriano, Xavi/Sanchez dk55, Song, Iniesta/Thiago dk64, Villa, Fabregas na Pedro.
Bayern Munich: Neuer, Lahm/Rafinha dk77, Boateng, Van Buyten, Alaba, Javi Martinez/Tymoschuk dk74, Schweinsteiger/Gustavo dk66, Robben, Muller, Ribery na Mandzukic.
Wembley, here we come: Arjen Robben (centre) celebrates after opening the scoring at the Nou Camp
Wembley, tunakuja: Arjen Robben (katikati) akishangilia baada ya kufunga bao la kwanza Nou Camp
Fussball's coming home: Bayern secured an all-German Champions league final against Borussia Dortmund
Fussball inakwenda nyumbani: Bayern imeungana na Wajerumani wenzao, Borussia Dortmund katika fainali
No stopping that: Robben (unseen) cut inside and curled a brilliant finish into the far corner of Barca's net
Hakuna kuzuia hiyo: Robben (haonekani) shuti lake likitinga nyavuni
Hamstrung: Lionel Messi (right) was left on the bench despite Barca's need to overturn a four-goal deficit
Nyama za paja: Lionel Messi (kulia) alibaki benchi licha ya Barca kutakiwa kupiku kipigo cha mabao manne
Hang your head: Barca goalkeeper Victor Valdes screams in frustration after Pique's gaffe
Kichwa chini: Kipa wa Barca, Victor Valdes akilalamika baada ya Pique kujifunga
Salt in the wounds: Bayern's Thomas Muller (centre left) headed in a third goal late on
Kwisha habari yao: Thomas Muller wa Bayern akifunga bao la tatu
London calling: Bayern Munich goalkeeper Manuel Neuer (left) and his team-mates have a final date
Wito wa London: Kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer (kushoto) na wachezaji wenzake wametinga fainali
What's gone wrong? Gerard Pique, David Villa and Cesc Fabregas were left scratching their heads
Tatizo nini? Gerard Pique, David Villa na Cesc Fabregas wakitafakari kipigo

No comments:

Post a Comment