POLISI WAREJESHA FEDHA KWA WACHINA
"Jamani pesa yenu iliyoibiwa hii
hapa," Ni kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Iringa ACP Athmani Mungi
akiwaonyesha raia wa China maburungutu ya fedha zilizonusurika kutoka
kwa majambazi waliowateka na kuwapora raia wa China.
Fedha shilingi Milioni 80 ambazo
zimerejeshwa na jeshi la polisi kutoka mikononi wa majambazi wa tukio la
utekaji wa raia wa Kichina, waliovamiwa katika mlima wa Nyang'olo
mkoani Iringa.
Kamanda Mungi akiwa ameshika Silaha
aina ya ShortgunGreener ambayo imekatwa Mtutu (kitako) silaha iliyotupwa
na watu wanaosadikika kuwa ni majambazi baada ya kuzidiwa nguvu na
askari polisi katika mapambano ya kuokoa fedha za raia wa China.
Mamilioni ya fedha yakiwa yameshikwa
na kamanda wa jeshi la Polisi mkoni Iringa, mara baada ya kusalimika
kutoka mikononi mwa majambazi, ambao walipora vitita vya fedha hizo
kutoka kwa raia wa China.
Raia wa China wakiwa na askari polisi
katika ukumbi wa ofisi ya kamanda wa jeshi la polisi wakipewa taarifa za
kupatikana kwa baadhi ya fedha zao na vifaa walivyoporwa na watu
wanaosadikika kuwa ni majambazi.(P.T)
No comments:
Post a Comment