MWENGE WA UHURU UPO DSM SASA
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Said
Meck Sadiki (kulia) akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Mkoa wa
Pwani na Skauti Mkuuwa Chama cha Skauti Tanzania Hajati Mwantum Mahiza
(kushoto) katika uwanja wa ndege wa Terminal one (1) leo Jijini Dar es
Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Mafia Sauda Salum
Mtondoo(kulia) akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani na
Skauti Mkuuwa Chama cha Skauti Tanzania Hajati Mwantum Mahiza (kushoto)
kwa ajili ya kuukabidhi Mwenge kwa Mkoa wa Dar es Salaam, katika
makabidhiano yaliyofanyika uwanja wa ndege wa Terminal one (1) leo
Jijini Dar es Salaam.(P.T)
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa
Juma Ali Simai akitoa salamu za shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani
Hajati Mwantum Mahiza (aliyevaa Miwani) kabla ya kuukabithi Mwenge huo
kwa Mkoa wa Dar es Salaam, katika makabidhiano yaliyofanyika uwanja wa
ndege wa Terminal one (1) leo Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu na Mkurugenzi wa
Idara ya Maendeleo ya Michezo Kutoka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni
na Michezo Leonard Thadeo(kushoto) akipokea Mwenge wa uhuru kutoka kwa
Mmoja wa wakimbiza mwenge kitaifa, katika uwanja wa ndege wa Terminal
one (1) leo Jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Said
Meck Sadiki akitoa taarifa fupi mara baada ya kupokea Mwege wa Uhuru leo
Jijini Dar es Salaam katika uwanja wa ndege wa Terminal one.
Picha na Hassan Silayo-MAELEZO
No comments:
Post a Comment