Sunday, August 4, 2013

YANGA FULL RAHA TAIFA

Mshambuliaji wa Yanga, Jerryson Tegete akiwa juu baada ya kuchezewa rafu wakati wa mechi ya Yanga na Mtibwa leo.
Said Bahanuzi (11) akishangilia  bao aliloifungia Yanga dakika ya 24 ya mchezo. Kulia ni Nadir Cannavaro (23).…
Mshambuliaji wa Yanga, Jerryson Tegete akiwa juu baada ya kuchezewa rafu wakati wa mechi ya Yanga na Mtibwa leo.
Said Bahanuzi (11) akishangilia  bao aliloifungia Yanga dakika ya 24 ya mchezo. Kulia ni Nadir Cannavaro (23).
Chuji kazini.
YANGA SC imeibuka kidedea kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mechi ya kirafiki iliyofanyika leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga yamefungwa na  Said Bahanuzi dakika ya 24, Jerryson Tegete dakika ya 80 na Hussein Javu katika dakika ya 87, wakati lile la Mtibwa lilifungwa na Shaban Kisiga dakika ya 57.
Kikosi cha Yanga kilikuwa hivi:
1.    Deogratius Munishi 'Dida' 2.Juma Abdul 3.Oscar Joshua 4.Nadir Haroub 'Cannavaro' 5.Issa Ngao 6.Athuman Idd 'Chuji' 7.Said Bahanuzi 8.Salum Telela 9.Jerson Tegete 10. Shaban Kondo na 11.Haruna Niyonzima.
Walioanzia benchi ni 1.Ally Mustapha 'Barthez' 2.Yusuph Abdul 3.Ibrahim Job 4.David Luhende 5.Rajab Zahir 6.Bakari Masoud 7.Hussein Javu 8.Abdallah Muhi 9.Nizar Khalfani na 10.Hamis Kiiza.
TASWIRA ZAIDI ZA MTANANGE HUO:
Hekaheka uwanjani.
Kikosi cha Yanga.
Kikosi cha Mtibwa Sugar.
Manahodha wakisalimiana kabla ya mechi.
Kocha Mkuu wa Yanga Ernie Brandts (wa kwanza kulia) na viongozi wenzake wakifuatilia mtanange huo.
Kocha wa Mtibwa Sugar, Meck Mexime (wa kwanza kushoto) na wenzake wakishuhudia mechi hiyo.
Bahanuzi akikwaana na mchezaji wa Mtibwa.
Vuta nikuvute wakati wa mechi hiyo.
(PICHA NA RICHARD

No comments:

Post a Comment