Thursday, August 22, 2013

WAVAMIA KUSAKA SAMSUNG FEKI K.KOO


Meza yetu  ya habari imepokea habari  toka Kariakoo zikitujuza Uvamizi wa gafla uliofanywa  kwa kushirikisha Polisi na Raia wa Kizungu   waliopita  kwenye maduka na kuchukua simu zote za  aina ya Samsung  za kichina.

Baada ya kufanya  mahojiano kwa njia ya mtandao na simu na baadhi ya wafanyabiashara, tulifahamishwa kuwa hii ni mara ya tatu na baadhi ya wafanyabiashara wamekiri kuwa huu ni mchezo mchafu  unaochezwa na baadhi ya Maaskali polisi wa Kituo cha Msimbazi......"

Kwa masharti ya kutotajwa jina mfanyabiashara mmoja alikuwa na haya ya kusema “yaani hawa  wazungu wamevamia hapa  na Askari na kuchukua simu za kichina za Samsung wakati sisi mzigo tunanunua china hivi  ni halali kweli ? Ujue Watanzania tunashushana na kutiana umaskini wenyewe kwa wenyewe ... hii ni mara ya tatu na kila wakija wanachukua mzigo wote hivi  ni kweli serikali haijui ? au  mpaka siku tuliwashe ndio watu watafutane  au  ijulikane? Au wanataka  waseme  tulianzisha vurugu , Raia wa kigeni aingie duka la mzalendo kupekua kweli jaman? Inauma sana unajua dada ?

No comments:

Post a Comment