Tuesday, July 16, 2013

SIMULIZI MAISHA YA OSAMA NA UJASUSI MPAKA KUUAWA

 
Na FUHRER wa JF
Taarifa za Osama zilitolewa na detainee watatu wa alqueda waliopo Guantanamo. wa kwanza ni Mastermind wa 9/11 Khaleed Sheikh Mohamed (KSM), huyu ndie alimtaja Courier wa Osama ajulikanaye kwa jina la Al Kuwait ambaye ndiye anaebeba maelekezo na mawasiliano yote kutoka kwa osama na kupeleka kwa foot soldiers, Wa pili kumtaja Al Kuwait ni Abu Zubeida, Huyu Abu zubeida pamoja na Ramzi Yousef ndio waliolipua WTC kabla ya 9/11. Abu zubeida kwanza aliteswa na CIA kwa kutumia Enhanced Interogation techniques kama water borne akagoma kutoa information yoyote, mpaka CIA wakamtishia kumkabidhi kwa intelligence ya Saudi Arabia wakiamini ataogopa maana Saudi Arabia wanajulikana kwa kutesa, wakashangaa anawaambia wampeleke Saudi. Hapo ndio CIA wakacheza trick wakampakiza kwenye ndege na kuzunguka naye muda mrefu angani wakijifanya wanampeleka Saudi Arabia mwisho wakatua naye sehemu hukohuko marekani wakawachukua maofisa wa CIA waarabu wakiwa na nguo za jeshi la Saudi Arabia wakaanza kumuuliza maswali hapo ndio akamtaja Al Kuwait, halafu akawataja wafadhili wa Osama akiwepo Mtoto wa mfalme wa Saudi, Generali wa Jeshi la Saudi na maofisa wengine wawili wa serikali ya Saudi na akawapa namba ya motto wa mfalme wampigie ili awaamrishe wamwachie. watu wote waliotajwa na Abu zubeida CIA waliwaua kuanzia mtoto wa mfalme alikutwa amekufa akiwa vacation, yule General wa jeshi alikutwa amekufa jangwani kwa kiu na kukosa maji na wale maofisa wote. Huo ndio ukawa mwanzo wa Osama kukosa hela (financial suffocation). wakaanza kumfuatilia Al Kuwait Pakistani wakamtrace akitokea sokoni hadi nyumba aliyokuwa akienda Abbottabad. Osama aliishiwa hela mpaka wake zake walikuwa wanaenda kwa sonara wanauza mikufu na herein zao ili wapate hela ya kula. Ndio CIA wakamkodia nyumba karibu na nyumba ya Osama Afisa wake aliyekuwa anafanya kazi katika Shirika la Save the Children ambalo lilikuwa linafanya kampeni ya kinga ya magonjwa ya watoto. Na sio kwamba eti marekani walikuwa wanachukua DNA za watoto na ku-match na za Osama huo ni uwongo kwa sababu kinga iliyokuwa inaratibiwa na Save the Children ilikuwa ni ya Matone sasa kuwapa watoto matone uta-extract vipi DNA. Aliyebaki sasa ni second in command wa alqaeda daktari wa Misri Ayman Al Zawahil ambaye naye inaaminika amejificha kwenye mpaka wa Afg na Pak.

========================================= MWENDELEZO=====
Vile vile katika ripoti hiyo ya commission inamtaja afisa mmoja wa shirika la kijasusi la Pakistani (ISI) kuwa kuna uwezekano alihusika katika njama za marekani kumkamata Osama kwa kuwa wiki moja kabla ya tukio la kumkamata Osama, aliwatuma watu kukata miti mikubwa iliyokuwa inazunguka ile nyumba Abbottabad ikiwa ni maandalizi ya helicopter kutua. Vile vile baada ya tukio la kukamatwa Osama aliuza vitu vyake na kuondoka Pakistani. Tofauti kati ya mashirika ya intelligence ya huku kwetu na nchi zilizoendelea ni kuwa wenzetu mashirika yao yanafanya mission zenye maslahi kwa taifa siyo kwa chama tawala. Ndio maana mission ikishakamilika wanatoa taarifa yote in detail kasoro baadhi tu ya tactics ambazo wanaona wataendelea kuzitumia kwenye mission nyingine. Huku kwetu mission zilizojaa TISS ni zile za kukandamiza Upinzani kama kumuua Kombe, kuua viongozi wa upinzani, kuwarushia mabomu Chadema n.k hizi mission hauwezi kuja kujua ukweli mpaka mmoja wao awageuke aropoke. Wenzetu mission zao zinakuwa high classified, lakini ikishakamilika tu wana-disclose kila kitu. Kwa mfano mission ya kumkamata Khaleed Sheikh Mohamed (KSM) the ring leader and mastermind wa 9/11 na akina Ramzi Yousef inajulikana ilifanywaje. Walifuatilia trail ya hela zote zilizokuwa wired kwenye account ya Mohamed Attar (kiongozi wa magaidi waliobamiza ndege WTC) Walianzia Dortimund Ujerumani ambakao Mohammed Attar alikuwa anasoma master of Science in Urban Planning katika chuo kikuu cha Dortimund. Walifuatilia trail ya ufadhili wa hela, msikiti aliokuwa anaswali hadi wakajua cell yao ilikuwa na kina nani, safari zake Pakistani na watu aliokuwa anakutana nao. Mohamed Attar ndio alikuwa ana-distribute hela kwa wale wengine za kusomea u-pilot wa ndege marekani. lakini hadi wanasomea upilot walikuwa hawajui mission yao itakuwaje. aliekuwa anajua mission ni KSM na Mohamed Attar. Kuna gaidi mmoja ambaye alikuwa yupo kwenye kikosi cha kwanza lakini alinyimwa viza ya kuingia marekani ndio alimtaja KSM kuwa ndie aliekuwa anawafadhili. Tofauti na kina Osama, KSM alikuwa anaishi maisha ya kifahari, anaingia kwenye club za usiku, anatumia vileo, anatumia simu, anachukua machangu, hakuwa anaishai maisha ya kiislamu. Kosa la kwanza na kubwa ambalo KSM na Ramzi walilifanya ni kumualika mwandishi wa habari wa Al-jazeera kwenda kuwahoji Pakistani. Ikieleweka kuwa kabla ya 9/11, Osama alikuwa anajulikana lakini hakuwa maarufu sana, hivyo kulikuwa na struggle kati ya magaidi kila mtu akitaka kupata umaarufu kuwa yeye ndio gaidi zaidi. Hiki ndicho kiliwasukuma KSM na Ramzi kumualika yule mtangazaji wa Al-jazeera kwenda kuwahoji. Yule mtangazaji alienda Islamabad akafungwa kitambaa usoni akazungushwa kwenye gari kuanzia asubuhi hadi jioni ili asijue muelekeo, mwishowe akashushwa kwenye gari wakamuingiza kwenye nyumba ambayo ina bunker alipofunguliwa kitambaa akakutana uso kwa uso na KSM akiwa na Ramzi Yousef. Pale KSM aka-declare jihad against American na ku-confess yeye ndiye aliyepanga na ku-finance mission nzima ya kubamiza ndege WTC. Yule mtangazaji wa Al-jazeera alipomaliza kuwahoji akaomba aondoke na Video footage wakamkatalia ila wakamruhusu achukue Audio record, hilo ndilo lilikuwa kosa kubwa sana maana ile audio iliporushwa tu Al-Jazeera, CIA wakaenda kuichukua Al-Jazeera wakatenganisha voice print za kila mtu alieongea kwenye ule mkutano wakaingiza kwenye mashine yao inayo-identify voice print ya kila mtu kama finger print. Hapo ndio ukawa mwanzo wa Drone attack Pakistani. Mtu akiongea kwenye simu kabla hajakata simu anashangaa bomu limeshatua. Kuna tukio moja walikuwa wamewasiliana wahudhurie harusi na Ayman Al Zawahil atakuwepo, machale yakawacheza Zawahili hakwenda, ile harusi ilibutuliwa na drone walikufa watu ukoo mzima. Baada ya kukamatwa Ramzi, KSM alistuka kuwa anafuatiliwa kwenye simu hivyo alikuwa hatumii simu yake, anaomba watu atumie simu zao ndio maana zoezi la kumkamata KSM lilishindikana zaidi ya mara 20, wakimtrace sehemu wakienda hawamkuti, alikuwa halali sehemu moja mara mbili mfululizo, Mpaka walipoamua kumtengenezea ramani kwa kutumia simu anazotumia, waka-identify sehemu 14 ambazo kuna uwezekano mkubwa wa kumkuta. Hizo sehemu zote zikafanyiwa kitu kinaitwa "synchronized ambush", yaani vikatengenezwa vikosi 14 vya askari wa Pakistani vikishirikisha maafisa wa CIA katika kila kikosi ambavyo vita-ambush sehemu zote 14 kwa muda mmoja, hapo ndipo walipomkamata KSM lakini walichoshangaa ni kuwa kwenye location moja katika zile 14 walikuta kiwanja hakina nyumba. walipofuatilia waya wa simu unaotumika kwa ID ya kiwanja hicho uko kwenye nyumba ipi ndipo ofisa wa ISI mtaalamu wa IT akai-trace nyumba inayotumia ID ya kile kiwanja humo ndipo walipomfurumusha na kumpiga risasi Abu Zubeida ambaye alipelekwa kutibiwa ujerumani akapona na kutoa siri kibao.

==============================================MWENDELEZO============
 Wakuu nitaendelea kuwapa simulizi hizi za mission za CIA, MOSSAD na KGB maana wenzetu wanaziweka wazi hawana cha kuficha kama bongo. Ile mission ya kumkamata Osama ni kali lakini kwa watu wanaojua mission zilizofanyika hapa duniani, hakuna mission kali kuizidi ile ya Entebbe iliyofanywa na MOSSAD, hata hii ya Osama ilichukua items nyingi kwenye mission ya Entebbe. Ukitaka kujua ile ya Entebbe ni kali kuliko ya Osama linganisha technologia zilizotumika, hii ya Osama walitumia chopa za shinoku zenye technology ya stealth inayoweza kukwepa rada wakati ya Entebbe hakukuwa na technology hiyo. Ndege zilizohusika kwenye mission ya Osama ziliruka kutoka kwenye military base ya marekani iliyopo Jalalabad Afg ambayo ipo ka 20 km kutoka kwenye mpaka na Pak wakati Ndege zilizohusika kwenye mission ya Entebbe ziliruka kutoka Tel Aviv kupita nchi mbili ambazo ni hostile Egypt na Sudan 5,000km kuja Entebbe. Operation ya Osama kulikuwepo na maofisa wa CIA waliokuwa kwenye ofisi ya ubalozi ambao walielekea Abbottabad mapema kwaajili ya ku-monitor situation na kuna maofisa wa ISI ambao walikuwa kwenye jeshi la Pakistani ambao walikuwa wanatoa taarifa kwa maofisa wa CIA kila kinachoendelea kuhusiana na response ya jeshi la Pakistani. Siku nikipata nafasi nitawasimulia ile operation ya Entebbe ilivyopangwa na failures na success zake. kama ilivyokuwa ya Osama zilipangwa plana 4 za kuifanya ile mission ya Osama na zote zilifanyiwa mazoezi ndio maana ile helicopter ilivyokosa thrust na kudondoka walibadili plan kutoka Plan A kwenda plan C, sasa siku nikipata nafasi nitawaeleza Plani A ilikuwa ikoje, plan b,c na d. Na kwa nini ile helicopter ilivyodondoka walibadili plan kutoa A kwenda C, kwa nini hawakuenda plan B.

================================================MWENDELEZO=========
 Uzuri wa hizi fact hata ukizibishia leo kuna sikuutazikubali tu, wewe uko huku Tanzania unabisha Osama hakuuwawa, wakati wakezake osama wanajulikana na watoto wa osama wanajulikana na wote wanathibitishawalikuwa na baba yao na ni kweli aliuwawa hivi tukuamini wewe ulioko hukuTanzania na stori zako za vijiweni. Wake zake osama walimkinga asipigwe risasina navy seals wakapigwa wao za miguuni na osama akapigwa risasi mbiliwanathibitisha kuwa ni kweli osama kauwawa, wewe huku Tz unabisha.

Halafu sikusema osama kakubali kuwa ndiye aliyepangamashambulizi ya WTC, aliyekubali kuwa yeye ndiyo brain behind 9/11 ni KSM naRamzi walipohojiwa na mwandishi wa Aljazeera. Wazo la kushambulia WTC halikuwala Osama ila lilikuwa la KSM ndio alimpelekea Osama wakati yupo Afg enzi zataleban. KSM alihitaji support kutoka kwa Osama ya foot soldiers wa kufanya ilemission na financial support. Na ile tactic ya kuzibamiza ndege kwenye majengo,KSM aliitoa kwenye vita kuu ya pili ambapo Japanese suicide pilots walikuwawanaruka na ndege zenye milipuko na kwenda kujibamiza kwenye manowari zamajeshi ya washirika na kuzizamisha, hii staili ilijulikana kama “kamikaze”,walifanikiwa kuzamisha manowari nyingi za kivita na kuuwa askari zaidi ya 5000wa majeshi ya washirika (alied troops). KSM aliona sifa za ile mission ya WTCzinaenda kwa Osama wakati lile lilikuwa wazo lake ndio maana akaamua kumwitaYule mwandishi wa Aljazeera ili kuweka record straight. Ukienda nchi za kiarabuwanaoitwa magaidi na marekani kule ni mashujaa (martyrs) ndio maana hata waowanaoneana wivu mwingine anapopata sifa kama unamkumbuka Abu Musab Al Zaqawialipata sifa sana wakati wa vita ya Iraqi maana ndiye aliyeongoza mapambano yaAlqaeda katika ukanda ule, sifa ziliongezeka zaidi pale alipomteka na kumchinjakama kuku askari wa marekani aliyekuwa anaendesha kifaru. Osama alipoona AlZaqawi anapata umaarufu sana akamuonya kuwa mambo anayoyafanya yanaenda kinyumena mafundisho ya kuran hivyo kabla hajafanya kitu chochote lazima aombe kibali kutokakwake. Lakini ukiangalia kilichomsukuma kutoa onyo kwa Zaqawi ni wivu kuwaatamzidi umaarufu maana kama ni kuchinja makafili (infidels) jeshi la mujahdeenla Afghan lililokuwa linaongozwa na kina Mular Omar na Osama ndilo lilikuwalinawachinja makafili na traitors kama unakumbuka Yule tribal lord wa NothernAlliance alivyokamatwa na kuchinjwa Ijumaa baada ya swala kule Kandahar wakatiwa uvamizi wa Marekani kule Afghanstan.

Issue ya doble agent inatumika sana katika hizimission ili ku-infiltrate enemy territory ingawa sometimes inback-fire.Successful mission mojawapo iliyotumia double agent ni ile iliyomuua yule imamwa yemen mzaliwa wa marekani Anwar Al Awlaki. Huyu alikuwa anatafutwa namarekani kwa kuhusika kwake na 9/11 ambapo ilikuja kujuikana kuwa hijackerswatatu wa 9/11 walikuwa wanasali kwenye msikiti wake. Vilevile moja waoalieongoza flight 77 alikuwa na namba yake kwenye diary yake. Huyu imamalikimbilia yemen akajificha huko. Kilichomponza ni kuwa mahubiri yake mengialikuwa anayapost kwenye U-tube mpaka kuna wakati CIA waliomba kibali congressili waondoe baadhi ya mahubiri yake yaliyokuwa yana-incite jihad kwenye utube.Sasa alipokuwa yemen CIA kwa kushirikiana na Danish Intelligence Agency PETwakam-recruit kijana mmoja wa denmak ajulikanaye kama Storm aende akazoeanenaye. Yule kijana akajifanya nye ni sympathizer wa jihadi akawa naye anachangiakwenye mahubiri anayotoa Anwar kwenye internet mwishowe akaenda yemen kukutanana Anwar. Anwar akamweleza kuwa anapanga kushambulia kwenye ma-supermarketmakubwa marekani kwa kutumia biological weapons. Baada ya mahusiano ya mudamrefu Anwar akamwomba amnunulie Flash am-downloadie magazeti ya marekani iliajue wanamwandikaje kwa kuwa yeye alikuwa mafichoni. Hapo ndipo CIA wakampaStorm flash disc yenye tracking micro-chip. Wiki moja tokea ampe ile flash CIAwalituma drone ikamuua akiwa kwenye gari na wenzake watatu baadae kakamuua namtoto wake.

Lakini hii technique yak u-recruit doble agent huwasometimes inaback-fire kwa sababu huwa subjected to loyality. Si unakumbukakule Afghanstani kwenye base ya marekani ya kupambana na mitandao ya kigaidi yaalqaeda, Haqqan na talebani inayojulikana kama CAMP CHAPMAN kilinuka mwaka2009. CIA na Jordanian Intelligency walim-recruit Jordanian doctor aliyekuwaanasympathize na Alqaeda aliyejulikana kama Humam Khalil Abu-Mulal al-Balawiakawa “TRIPLE AGENT”, Huyu anatoka kijiji kimoja na Alqaeda leader inMesopotamia Abu Musab Al Zarqawi. Sasa Al Balawi alifanya kazi na CIA na kuwapataarifa za ukweli walipo wapiganaji wa Alqaeda na ikawa ni kweli CIA wakitumadrone inawaua. Si wakamwamini, akawaambia yeye atawafanikishia CIA kumuua aukumkamata Ayman Al Zawahil, CIA wakaingia mkenge akawa akiingia kwenye base yaoya chapman hawamsachi. Siku akawadanganya anataarifa muhimu sana kuhusiana naAl Zawahil hivyo anahitaji kuonana na top officials wa CIA, Basi yule mamaambaye alikuwa Chief of operation katika ile base anaitwa Jennifer Lynne Matthews akawaita hadimaafisa wengine wa CIA kutoka Kabul, alipofika getini hakusachiwa ingawa kunamageti matatu, maofisa wote wakatoka kumpokea nje, kumbe kajifunga bomu la kilo15 akalilipua aliua watu 9 palepale na wengine kadhaa kujeruhiwa. Hii ndio riskya ku-recruit double agent hauwezi kujua loyality yake ipo kwa nani. Mara baadaya kujitoa muhanga na kuuwa maofisa wa CIA, Al Balawi alionekana kwenye videofootage iliyorushwa kwenye channel za TV Pakistani akiongea kuwa amefanya liletukioa kama kulipiza kisasi cha kiongozi wa Alqaeda Pakistani Baitullah Mehsud aliyeuwawa na CIA kwa drone

No comments:

Post a Comment