FUVU la kichwa cha binadamu, limekutwa likiwa limeficha juu ya dari
katika nyumba ya mtu mmoja wilayani Same mkoani Kilimanjaro, kutokana na
imani za kishirikina. Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema tukio hilo, lilitokea
Julai 17, mwaka huu saa 8:17 mchana katika Kijiji cha Mbono.
Alisema askari waliokuwa wakisaka wauzaji wa gongo na bangi,
walipekuwa nyumba ya Saidi Fundi (43) na kukuta fuvu la kichwa cha
binadamu, likiwa limeficha juu ya dari katika nyumba yake.
Alisema
baada ya mahojiano baina ya askari na mtuhumiwa huyo, alisema fuvu hilo
ni la baba yake mzazi, Hamisi Elidina aliyefariki dunia miaka ya 1970
na kuzikwa katika eneo la Kifaru wilayani Mwanga.
Alisema
mtuhumiwa huyo, alifikia uamuzi wa kufukua kaburi la baba yake kutokana
na maagizo ya mizimu ya ukoo wao, kuwa akifanya hivyo atakuwa na maisha
mazuri.
Alisema kutokana na tukio hilo, uchunguzi unaendelea ili kubaini kama ni kweli fuvu hilo ni la binadamu.
Alisema
baada ya uchunguzi huo kukamilika, mtuhumiwa huyo atafikishwa
mahakamani kujibu mashtaka yanayomkabili, kwani kukutwa na kiungo
chochote cha binadamu ni kosa kisheria.
No comments:
Post a Comment